logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Martha Karua atangaza kumuunga mkono Raila Odinga

Martha Karua ametangaza kumuunga mkono Raila Odinga katika uchaguzi wa Agosti 9.

image
na Radio Jambo

Burudani23 March 2022 - 11:45

Muhtasari


• Kinara wa NARC- Kenya Martha Karua hatimaye amuunga mkono Raila Odinga kwa uchaguzi wa Agosti 9.

• Hatua hii inajiri baada ya vinara wengine wa muungano wa OKA kujiunga na vuguvugu la Azimio.

Star

Kinara wa chama cha Narc Kenya Martha Karua ametangaza kumuunga mkono kiongozi wa muungano wa Azimio la Umoja, Raila Odinga katika uchaguzi wa Agosti 9.

"Kutoka leo NARC- Kenya na mimi mwenyewe tunamuunga mkono Raila Odinga," Karua alisema.

Aliongeza kwamba Raila Odinga amepigania ukombozi wa taifa hili na kwamba yeye tu ndiye aliye na uwezo wa kupeleka taifa la Kenya mbele.

Aidha alisema kwamba NARC Kenya itamfanyia Raila Odinga kampeni katika maeneo yote ya taifa ili kuuza sera zake.

Karua ambaye siku ya Jumanne alitangaza kwamba muungano wa OKA ulikuwa umesambaratika hasa baaada ya vinara Kalonzo Musyoka wa Wpier, Gideon Moi wa Kanu na Cyrus Jirongo wa UDP kujiunga na muungano wa Azimio, alisema Raila ndiye kiongozi anayeweza kuliongoza taifa hili.

Akitangaza kuvunjwa kwa muungano wa OKA siku ya Jumanne, Karua alisema kwamba chama chake kingemuunga mkono tu kiongozi ambaye ana historia pana ya ukombozi wa taifa, mzalendo na muadilifu.

Kwa upande wake Raila Odinga alisema kwamba atahakikisha Karua amepata nafasi katika vuguvugu la Azimio la Umoja.

Akimtaja Karua kama kiongozi ambaye amepitia changamoto nyingi kupigania taifa hili, Raila alimpongeza kwa kufanya uamuzi mzuri kuungana naye.

Raila alisema kwamba hiyo ilikuwa fursa nzuri kwa wawili hao kuungana kwa mara nyingine  tena ili kuhakikisha wanaleta maendeleo katika taifa hili na kuwakomboa wakenya.

 

 

 

Kabla ya kukutana na Karua, kinara wa ODM Raiola Odinga alikuwa amehudhuria mkutano wa wajumbe wa chama cha UPIA.  Chama hicho kilitangaza kuunga mkono azma ya Raila Odinga.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved