logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kalonzo amelazimishwa kujiunga na Azimio-Jimi Wanjigi adai

Aliongeza kuwa tofauti zake na Waziri Mkuu wa zamani na Rais sio za kibinafsi.

image
na Radio Jambo

Habari29 March 2022 - 08:45

Muhtasari


  • Mwanasiasa Jimi Wanjigi amesema kuwa kinara wa ODM Raila Odinga ndiye aliyemshauri kujiunga na siasa

Mwanasiasa Jimi Wanjigi amesema kuwa kinara wa ODM Raila Odinga ndiye aliyemshauri kujiunga na siasa.

Akizungumza Jumatatu, Wanjigi alisema kuwa wakati huo, Waziri Mkuu huyo wa zamani alimweleza kuwa anastaafu kutoka kwa siasa.

“Raila alinishauri nijiunge na siasa, akasema anastaafu, akaniambia kuwa ameisaidia nchi vya kutosha na ni wakati wa kizazi kingine kuchukua hatamu, sijui ni nani, lakini nadhani kuna mtu anamsukuma. " aliiambia NTV.

Mfanyibiashara ambaye hivi majuzi aliidhinishwa kuwania urais kwa tiketi ya chama cha Safina alisema alitofautiana na Raila baada ya chama kumtenga.

Aliongeza kuwa tofauti zake na Waziri Mkuu wa zamani na Rais sio za kibinafsi.

Wakati wa mahojiano, Wanjigi alimshutumu kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka kwa kulazimishwa kufanya kazi na Raila chini ya muungano wake wa Azimio la Umoja.

"Niliwekwa kando na ODM nikaenda kwa rafiki yangu Kalonzo ambaye tulikuwa naye 2017. Tulipokuwa Kitui aliniomba nisimpeleke tena Azimio au Raila Odinga. Ninavyoona analazimishwa kufanya kazi na Azimio, namfahamu."

Wanjigi pia alimshutumu Rais Uhuru Kenyatta kwa kutumia watu wengine kurefusha muda wake mamlakani zaidi ya 2022.

"Tumeandaliwa kwa miaka 60 iliyopita na ni wakati wa wananchi kujipanga. Raila na Ruto wamekuwa kwenye siasa kwa miaka 30 na tumeona walichofanya. Watu wanateseka."

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved