logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Azimio watabwagwa na UDA iwapo hawatapunguza wagombea - Herman Manyora

Herman Manyora awataka Azimio kupunguza idadi ya wagombea ili kuishinda UDA.

image
na Radio Jambo

Habari30 March 2022 - 05:33

Muhtasari


• Herman Manyora amesema kwamba Azimio watashindwa na UDA iwapo hawatapunguza idadi ya wagombea.

• Amewataka kufaya maamuzi ya busara ili kuepuka fedheha hiyo.

Star, KWA HISANI

Mchanganuzi wa masuala ya kisiasa, Herman Manyora amesema kwamba huenda muungano wa Azimio la Umoja ukabwagwa na chama cha UDA katika uchaguzi wa Agosti 9, iwapo hawatapunguza idadi ya wagombea.

Akizungumza kupitia video aliyopakia katika akauti yake ya Youtube, aliwataka Azimio kubadilisha mbinu zao ili kuhakikisha wamepata ushidi katika maeneo mbalimbali nchini.

Manyora alisema kwamba uwepo wa vyama vingi chini ya mwavuli wa Azimio utasababisha kugawanya kura zao hivyo kutoa mwanya kwa UDA kuibuka kidedea.

"Unajua Azimio ina vyama vingi na watu wengi wanataka kugombea , wasipochunga na wapige hesabu zao vizuri watashindwa na UDA," Manyora alisema.

Alisema licha ya Raila Odinga kuwa na sapoti ya rais Uhuru Keyatta, anapaswa kuhakikisha wanafaya majadiliano na wagombea mbalimbali ili kuhakikisha yule ambaye ni maarufu zaidi anawawakilisha katika ngome zao.

Aidha, hakusita kuweka wazi kuwa naibu rais William Ruto ana ushawishi mkubwa katika sehemu nyingi za taifa hivyo haitakuwa rahisi kwao kumpiku.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved