logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Acha matakwa ya kipuuzi!" Seneta Ole Kina amzomea Kalonzo kutaka kuwa mgombea mwenza wa Raila

Seneta Ole Kina kwa Kalonzo: Acha matakwa yako hayo ya kipuuzi. Tuoneshe kura.

image
na Radio Jambo

Habari19 April 2022 - 06:41

Muhtasari


• Seneta wa Narok Ledama Ole Kina amemtaka Kalonzo aache matakwa ya kipuuzi na badala yake kuwaonesha kura.

• Alisema mtu yeyote anayetaka kuwa mgombea mwenza wa Raila sharti aoneshe ubabe wake katika kuvutia kura.

LEDAMA 2

Seneta wa Narok Ledama Ole Kina amewasuta wale wanaong’ang’ania nafasi ya kuwa mgombea mwenza wa kinara wa Azimio-One Kenya, Raila Odinga huku wakitoa masharti makali wakitaka kupewa hiyo nafasi.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Ole Kina aliwasuta vikali na kuwaambia waache vipindi kwani watu wenye fikira za kusonga mbele sasa hivi wanasakanya kura na si kutoa vitisho kuhusu nini watafanya iwapo watanyimwa nafasi ya kuwa mgombea mwenza wa Raila.

Akionekana kumtupia vumbi machoni kinara wa chama cha Wiper, Kalonzo Musyoka ambaye amekuwa akitoa masharti makali akitaka kupewa nafasi hiyo, Ole Kina alimtaka awaoneshe kura na kumuambia kwamba wakenya wenye fikira za mbele hawatomsikiliza.

“Yeyote anayetaka kuwa mgombea mwenza wa Raila lazima atuoneshe ubabe wake kwa kuwavutia wapiga kura nchini kote kwa kutumia masuala yanayowakumba. Haya mambo ya kujihisi unafaa ni ushauri potofu. Tunataka watu wenye fikra za mbele, walio tayari kujitolea kwa Kenya, tuwache vipindi. Acha matakwa yako hayo ya kipuuzi. Tuoneshe kura. Wakenya wenye kusonga mbele hawatakusikiliza…sisi twasonga mbele,” aliandika Ole Kina.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved