logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ulifanya mazungumzo na Rais Kenyatta sio Raila, Elachi amsuta Kalonzo

Elachi amemsuta Kalonzo kwa kutaka nafasi ya ugombea mwenza akisema alifanya mazungumzo na rais wala sio Odinga.

image
na Radio Jambo

Habari19 April 2022 - 10:09

Muhtasari


• Beatrice Elachi ametupilia mbali madai kwamba Kalonzo alifanya mazungumzo na Raila Odinga.

• Alisema kwamba Kalonzo hapaswi kulazimisha Odinga kumpa wadhfa wa mhgombea mwenza.

Katibu mkuu mwandamizi katika kitengo cha jinsia ya umma, Beatrice Elachi.

Aliyekuwa spika wa Kaunti ya Nairobi Beatrice Elachi amemkashifu Kiongozi wa Chama cha Wiper Kalonzo Musyoka kuhusu kile alichodai kuwa alimvuta kiongozi  wa ODM Raila Odinga kwenye makubaliano ambayo hakuhusika kwayo.

Katika mahojiano na  runinga ya K24 Jumanne, Elachi alisema mazungumzo kati ya Kalonzo na Rais Uhuru Kenyatta hayakumhusisha Raila.

"Kalonzo alikaa na Rais na kujadiliana na sio na Waziri Mkuu wa zamani," Elachi alisema.

Zaidi ya hayo, alitilia shaka makubaliano kati ya Kalonzo na Rais Kenyatta.

“Kalonzo alisema hawezi kujadiliana na Raila na hivyo akafanya mazungumzo na Rais. Mkataba gani huu uliokuwa nao na Rais? Unamvuta Raila katika kitu ambacho hakuwahi kushiriki,” Elachi alisema.

Elachi alisema Kalonzo alifaa kujiunga na muungano wa Azimio la Umoja kwa mikono safi na kufanya kazi kwa ushirikiano  ili kuhakikisha Raila anakuwa rais ajaye, badala ya kung'ang'ania mdahalo wa mgombea mwenza.

Kalonzo katika siku za hivi majuzi ametangaza nia yake katika nafasi ya mgombea mwenza kabla ya uchaguzi mkuu wa Agosti 9.

Mnamo Jumatatu, Musyoka aliomba kanisa limwombee anapopigania nafasi hiyo katika Vuguvugu la Azimio la Umoja.

Kalonzo alidai baadhi ya watu wanapanga  njama usiku kucha kumfungia nje ya wadhifa huo  huku wadhifa huo unaoongozwa na Raila Odinga ukitaka kuunda serikali ijayo.

"Wanahangaika kupanga njama nani atakuwa mgombea mwenza na nani hatakuwa mgombea mwenza. Tafadhali wasaidie kubadilika na kujua kwamba alichokusudia Mungu hakuna mwanadamu atakayekizuia."

Alijiamini kuwa mapenzi ya Mungu yatatawala na atakuwa mgombea mwenza wa Raila kama ilivyokuwa 2013 na 2017.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved