logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+Video) Mwanasiasa wa UDA ajipata matatani kwa kuwatupia watu vipande vya keki 'kama kuku'

Muratha amekosolewa sana kufuatia video hiyo.

image
na Radio Jambo

Habari03 May 2022 - 13:22

Muhtasari


•Wamuratha alirekodiwa akitupia watu  vipande vya keki kama jinsi mfugaji anavyowatupia kuku wake mahindi.

•Muratha amekosolewa sana kufuatia video hiyo huku wanamitandao wengi wakionekana kughadhabishwa na kitendo chake.

Mpeperusha bendera ya UDA katika kinyang'anyiro cha uwakilishi wa wanawake wa Kiambu, Anne Wamuratha amejipata matatani baada ya video yake akitupia umati wa watu vipande vya keki kusambaa mitandaoni.

Katika video hiyo iliyorekodiwa katika uwanja wa Ruiru, Wamuratha anaonekena akitupia watu  vipande vya keki kama jinsi mfugaji anavyowatupia kuku wake mahindi. Watu waliokuwa wamejumuika pale wanaonekana wakiinua mikono yao juu katika juhudu za kufikia vipande vile vya keki.

Kabla ya kuanza kutupa keki ile, mtaalamu huyo wa masuala ya ndoa alisikika akiwaagiza wakazi wajipange vizuri ili kila mmoja aweze kufikiwa na kipande angalau.

Muratha amekosolewa sana kufuatia video hiyo huku wanamitandao wengi wakionekana kughadhabishwa na kitendo chake.

Video hiyo imekuwa ikivuma hasa katika mtandao wa Twitter ambako mamia ya Wakenya wamejitokeza kueleza ghadhabu yao.

Haya hapa baadhi ya maoni ya Wakenya:-

@paulinenjoroge Mgombea kiti cha mwakilishi wa wanawake wa Kiambu kwa tikiti ya UDA Wamuratha akishiriki mpango wa kupatia kuku chakula.. oops nilimaanisha kupatia mpango wa kupatiana keki.

@CaxstomePkigata Mgombea kiti cha mwakilishi wa wanawake wa Kiambu kwa tikiti ya UDA Anne Muratha anaonekana akitupa chakula kwa watu wenzake wa Kiambu katika uwanja wa Ruiru kama kwamba anapatia kuku chakula. Hii inatiua uchungu, inadhalilisha na ni kukosa utu.

@pterkarnja Mgombea kiti cha mwakilishi wa wanawake wa Kiambu kwa tikiti ya UDA Wamuratha amefanikiwa kutojipigia debe. Alikuwa anafikiria nini?? Acha aombe ushauri kwa gavana wa zamani. Atahitaji bahati kubwa.

@DrJuma_M Hiivideo ya Wamuratha inasumbua sana.

Anne Muratha alishinda tikiti ya UDA katika kura ya mchujo iliyofanyika mwezi jana. Aliwabwaga wanawake wengine wakiwemo mwanamuziki Loise Kim, mwanasaikolojia  Gladys Chania, MCA mteule Serah Kamunyi, Grace Wanjiku, Njeri Bakari, Pauline Agondoa, Juliet Wainaina na Mercy Nungari.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved