logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Junet:Kwa nini ni lazima Azimio kumhoji mgombea mwenza wa Raila

Jopo hilo linajumuisha makasisi na wawakilishi wa vyama vya siasa.

image
na Radio Jambo

Burudani04 May 2022 - 08:31

Muhtasari


  • Mnamo Aprili 27, Raila alitangaza jopo la wanachama saba kuwachunguza wale wanaotaka kuwania nafasi ya mgombea mwenza
JUNET.jfif

Katibu mkuu wa baraza la Muungano wa Azimio la Umoja-One Kenya Alliance Junet Mohamed amefichua ni kwa nini muungano huo lazima umhoji mtu ambaye atakuwa naibu wa Raila Odinga kabla ya uchaguzi wa Agosti 9.

Katika ujumbe wake wa Twitter siku ya Jumanne, Mbunge huyo wa Suna Mashariki alisema kwamba sababu kuu ambayo itawabidi kuwachunguza watu wanaotarajiwa kuwa wagombea ni kwa sababu hawataki kuishia na mtu kama naibu rais wa sasa.

"Kanuni inayoongoza katika kutambua mgombea mwenza wa mgombea Urais wa Azimio ni kwamba, hatutaki kuwa na naibu wa rais kama William Ruto," Junet alisema.

Matamshi yake yanakuja huku kukiwa na maswali kuhusu ni kwa nini wawaniaji wenza wa Raila Odinga wanapaswa kuchunguzwa na kuhojiwa.

Kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka ni miongoni mwa walioibua hoja kuhusu uamuzi huo, akisisitiza kuwa amemteua Raila mara mbili, 2013 na 2017, na amehudumu kama Makamu wa Rais wa Kenya kwa miaka mitano.

“Suala hili limeanza kunilemea sana. Naona kama jambo lisilokubalika kulijadili... Suala hili likitatuliwa mapema, litawapa baadhi yetu msukumo wa kampeni,” Kalonzo alisema wiki jana.

Mnamo Aprili 27, Raila alitangaza jopo la wanachama saba kuwachunguza wale wanaotaka kuwania nafasi ya mgombea mwenza.

Jopo hilo linajumuisha makasisi na wawakilishi wa vyama vya siasa.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved