logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanasiasa wanaotaka kuwa naibu wa Raila wapewa masaa 24 kuwasilisha maombi

Jopo limesema watamchagua naibu wa Raila kutoka vyama vinavyounda muungano wa Azimio.

image
na

Yanayojiri04 May 2022 - 11:06

Muhtasari


•Kamati hiyo ilisema watamchagua naibu wa Raila kutoka vyama vinavyounda muungano wa Azimio.

Jopo lililotwikwa jukumu la kutafuta mgombea mwenza wa kinara wa ODM Raila Odinga limewapa wale wanaomezea mate nafasi hiyo masaa 24  kutuma maombi yao.

Jopo hilo mnamo Alhamisi lilivitaka vyama 26 vya kisiasa vya Azimio kuwasilisha majina ya wanaopendekezwa kwa timu inayoongozwa na aliyekuwa Mbunge wa Kwanza, Noah Wekesa.

“Kamati inaomba wanachama wowote wa muungano wa Azimio La Umoja-One Kenya wanaotaka kuteua mtu yeyote kwa ajili ya kuzingatiwa kama mgombeaji wa nafasi ya Naibu Rais wa muungano huu kuwasilisha majina yao kabla ya kufungwa kwa shughuli za kesho, Alhamisi. , Aprili 5, 2022," Wekesa alisema.

Kamati hiyo ilisema watamchagua naibu wa Raila kutoka vyama vinavyounda muungano wa Azimio.

"Kamati itazingatia tu wagombeaji ambao ni wanachama wa vyama vinavyounda Muungano wa Azimio La Umoja One Kenya," Wekesa aliongeza.

Katika kile kinachoonekana kama kupunguzwa kwa matakwa ya awali ya kusaili wawaniaji wa nafasi hiyo, Kamati ilifafanua kuwa wagombea wanaotaka kujitokeza na kutoa mada mbele ya jopo la wajumbe ndio watakaoruhusiwa kufanya hivyo.

(Utafsiri: Samuel Maina)


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved