logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gavana Mutua agura Azimio na kujiunga na Kenya Kwanza

•Gavana Alfred Mutua ametangaza kuwa chama chake kimehamia kwenye muungano unaoongozwa na naibu rais William Ruto wa Kenya Kwanza.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri09 May 2022 - 07:41

Muhtasari


•Gavana Alfred Mutua ametangaza kuwa chama chake kimehamia kwenye muungano unaoongozwa na naibu rais William Ruto wa Kenya Kwanza.

Gavana wa Machakos Alfred Mutua

Chama cha Maendeleo Chap Chap kimejiondoa kwenye muungano wa Azimio La Umoja unaoongozwa na Raila Odinga na rais Kenyatta.

Gavana Alfred Mutua ametangaza kuwa chama chake kimehamia kwenye muungano unaoongozwa na naibu rais William Ruto wa Kenya Kwanza.

Akihutubia waandishi wa habari Jumatatu, Mutua amesema alitia saini mkataba na muungano wa Kenya Kwanza jioni ya Jumapili.

"Naibu Rais William Ruto ni mtu mzuri na ataibadilisha nchi hii. Jana usiku (Jumapili) tulitia saini mkataba na Kenya Kwanza na nakala hii hapa," Mutua alisema.

Mnamo Ijumaa, Mutua alidai kuwa Msajili na Muungano wa Azimio La Umoja-One Kenya walikataa kuwapa nakala ya mkataba wa muungano wa Azimio.

Hapo awali kiongozi wa chama cha Ford Kenya Moses Wetang'ula alikuwa amewakaribisha Mutua na Amason Kingi wa PAA kwenye muungano wao.

Wetangula aliwapongeza wawili hao kwa hatua waliyopiga  na kusema itaongeza muungano huo nguvu tunapokaribia uchaguzi mkuu.

"Hongera vyama vya siasa vya Maendeleo Chap Chap na PAA kwa kujiunga na Muungano wa Muungano wa Kenya Kwanza. Nguvu yenu inaleta nguvu zaidi na inatuhakikishia  ushindi wa Kenya Kwanza Alliance katika uchaguzi Mkuu wa Agosti 9. Hongera," alisema.

Kingi hata hivyo bado hajatoa matamshi yake rasmi kuhusu suala hilo.

Mutua na Kingi wamekuwa wakilalamikia kutengwa katika muungano wa Azimio.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved