logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kalonzo abadili msimamo na kufika mbele ya jopo la kutafuta mgombea mwenza wa Raila

Aliingizwa katika chumba cha mahojiano na Katibu wa jopo Elizabeth Meyo.

image
na Radio Jambo

Habari10 May 2022 - 06:32

Muhtasari


• Msimamo huu mpya wa Kalonzo unajiri siku moja tu baada ya mwenyekiti wa Kanu Gideon Moi kujiondoa kwenye mahojiano na kutangaza kumuunga mkono kinara huyo wa Wiper.

Katibu wa jopo la mgombea mwenza wa Azimio Elizabeth Meyo, kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka na Wakili Paul Mwangi wakimsindikiza Kalonzo kufika mbele ya jopo katika hoteli ya Serena mnamo Mei 10,2022.Picha/Enos Teche.

Kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka amebadili msimamo wake wa awali na kufika mbele ya jopo la kuwahoji wanaotaka nafasi ya mgombea mwenza wa Raila Odinga katika muungano wa chama cha Azimio – one Kenya.

Makamu huyo wa rais wa zamani siku ya Jumanne aliweka kando vitisho vyake vya awali kuwa hawezi kufika mbele ya jopo hilo na kuwasili katika Hoteli ya Serena mwendo wa saa tatu asubuhi.

Aliingizwa katika chumba cha mahojiano na Katibu wa jopo hilo Elizabeth Meyo na mshauri wa kisheria wa Kamati hiyo Paul Mwangi.

Msimamo huu mpya wa Kalonzo unajiri siku moja tu baada ya mwenyekiti wa Kanu Gideon Moi kujiondoa kwenye mahojiano na kutangaza kumuunga mkono kinara huyo wa Wiper.

Maswali ambayo jopo hilo linauliza ni pamoja na; uzoefu wa kisiasa wa mtu, sifa za kitaaluma na maswali ya jumla kuhusu jinsi ya kukabiliana na changamoto za kitaifa kama vile rushwa na ukosefu wa ajira kwa vijana.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved