logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ngirici amtaja aliyekuwa kamishna msaidizi wa KRA Wanjao kama mgombea mwenza

Ngige anatoka eneo bunge la Ndia.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri14 May 2022 - 14:21

Muhtasari


  • Ngirici alijiondoa katika UDA ya Naibu Rais William Ruto na kuwa mgombea binafsi, akitaja upendeleo

Mwakilishi wa Wanawake wa Kirinyaga, Wangui Ngirici, amemtaja aliyekuwa msaidizi wa kamishna wa KRA Eliud Wanjao Ngige kuwa mgombea mwenza katika kinyang'anyiro cha kiti cha ugavana.

Ngige anatoka eneo bunge la Ndia.

Ngirici alijiondoa katika UDA ya Naibu Rais William Ruto na kuwa mgombea binafsi, akitaja upendeleo.

Mwakilishi huyo wa Kike alidai kuwa licha ya kuwa miongoni mwa wafuasi wa awali wa Ruto, Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru alipendelewa kwa tikiti ya UDA.

Ngirici alizua gumzo alipotoa kauli mbiu yake ya kampeni iliyopewa jina la 'Smairo ni tiki' na alama yake iliyoangazia picha ya meno yake halisi.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved