logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wagombea urais waanza kuwasilisha hati za uteuzi kwa IEBC

Zoezi hilo linafanyika Bomas of Kenya kati ya Mei 29, 2022 na Juni 6, 2022.

image
na Radio Jambo

Habari29 May 2022 - 12:05

Muhtasari


  • Wagombea urais waanza kuwasilisha hati za uteuzi kwa IEBC

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka imeanza zoezi la kuwaidhinisha wawaniaji urais katika uchaguzi wa Agosti 9.

Zoezi hilo linafanyika Bomas of Kenya kati ya Mei 29, 2022 na Juni 6, 2022.

Katika ratiba iliyotolewa na Tume hiyo, Peter Kingori na Justus Juma wameratibiwa kuwasilisha karatasi zao za uteuzi kwa IEBC Mei 29, 2022 huku Prof George Wajackoyah na Peter Mongare wakitarajiwa kufika Mei 30, 2022.

Dorothy Kemunto atawasilisha stakabadhi zake Mei 31, 2022. Wengine ni Gibson Nganga (Juni 1), James Kamau (Juni 2), Jeremiah Nyagah, Jane Munyeki na David Mwaure Waihiga (Juni 3).

Mgombea urais wa Kenya Kwanza William Ruto na kiongozi wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka wameratibiwa kuwasilisha karatasi zao Juni 4, 2022.

Mgombea urais wa Chama cha Muungano Azimio One Kenya Raila Odinga anatarajiwa kuwasilisha stakabadhi zake mnamo Juni 5, 2022.

Dkt Ekuru Aukot na George Munyottah pia wamepangwa kushiriki Juni 5, 2022. Jimi Wanjigi, Muthiora Kiriara na Njeri Kathangu wanatarajiwa Bomas mnamo Juni 6, 2022.

Baada ya kupitishwa, wagombea urais sasa wako huru kufanya kampeni kabla ya uchaguzi.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved