logo

NOW ON AIR

Listen in Live

IEBC imekataa ombi la Prof. Wajackoyah la kutaka kibali cha kuwa mgombea Urais Agosti

Wakili huyo alikuwa na orodha kamili ya wafuasi kutoka kaunti 17 kati ya 24 zinazohitajika.

image
na Radio Jambo

Habari30 May 2022 - 11:56

Muhtasari


  • IEBC imekataa ombi la Prof. Wajackoyah la kutaka kibali cha kuwa mgombea Urais Agosti

Mgombea urais wa Chama cha Roots George Wajackoyah amekataliwa na IEBC kwa kukosa kuwasilisha idadi inayohitajika ya saini za wafuasi.

Wakili huyo alikuwa na orodha kamili ya wafuasi kutoka kaunti 17 kati ya 24 zinazohitajika.

Alikuwa miongoni mwa wagombea waliotazamiwa kukutana na Msimamizi wa Kitaifa Wafula Chebukati Jumatatu, katika ukumbi wa Bomas of Kenya.

"Mwenyekiti wa IEBC, Bw Wafula Chebukati amekataa ombi la Prof. Wajackoyah la kutaka kibali cha kuwa mgombea Urais kwa kukosa kuweka sahihi 2,000 zinazohitajika kwa kila kaunti katika angalau kaunti 24. Prof. Wajackoyah ana hadi tarehe 2 Juni saa 3 asubuhi. kukidhi hitaji hilo," IEBC Ilisema JUmatatu.

Wajackoyah ana hadi Alhamisi kuwasilisha sahihi kutoka kwa kaunti saba zilizosalia.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved