logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kalonzo apiga U-turn ya mwaka na kurejea kwa Azimio one Kenya

Kalonzo alisema kwamba amekuwa na muda wa kutosha kutafakari kuhusu hatima yake katika siasa.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri02 June 2022 - 11:27

Muhtasari


• Kinara huyo wa Wiper alisema kwamba azma yake sasa ni kuunganisha taifa la Kenya.

• Alisema ataunga mkono kwa dhati uteuzi wa Martha Karua kama mgombea mwenza wa Raila Odinga na atakuwa katika mstari wa mbele kupigia debe muungano wa Azimio.

Kinara wa Wiper Kaonzo Musyoka amerejea tena katika muungano wa Azimio One Kenya.

Akizungumza baada ya kukutanza na maafisa wa chama cha Wiper siku ya Alhamisi Kalonzo alisema kuwa baada ya kutafakari na kushauriana na wandani wake ameamuka kumuunga mkono kinara wa ODM Raila Odinga.

Kalonzo alisema kwamba amekuwa na muda wa kutosha kutafakari kuhusu hatima yake katika siasa.

“Nimeamua kuahirisha azma yangu kuwa rais wa Kenya kwa manufaa ya taifa,” Kalonzo alisema.

Kalonzo aliongeza kuwa…“Baada ya mashauriano ya kina nimekubali kwa unyenyekevu wadhifa wa waziri mkuu chini ya serikali ya Azimio One Kenya’

Makamu huyo wa rais wa Zamani alisema ataunga mkono kwa dhati uteuzi wa Martha Karua kama mgombea mwenza wa Raila Odinga na atakuwa katika mstari wa mbele kupigia debe muungano wa Azimio.

Kinara huyo wa Wiper alisema kwamba azma yake sasa ni kuunganisha taifa la Kenya.

Makamu huyo wa rais wa zamani alimshukuru mwenyekiti wa Kanu Gideon Moi kwa kusalia naye wakati huu wote alipokuwa akitafakari kuhusu mwelekeo wake mpya kisiasa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved