logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DP Ruto hatimaye aidhinishwa kuwania urais na IEBC

Ruto aliishukuru IEBC kwa jukumu lao la kuhakikisha Wakenya wanafanya uchaguzi wa kuaminika

image
na

Yanayojiri04 June 2022 - 09:10

Muhtasari


•Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alitangaza hayo Jumamosi baada ya Ruto na mgombea mwenza wake Rigathi Gachagua kuwasilisha stakabadhi zinazohitajika.

•Kwa vyombo vya habari, DP alisema ni wakati wao kuwa waadilifu na wenye usawa wakati wa kuripoti kampeni za kisiasa kabla ya uchaguzi.

Naibu rais William Ruto

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC)imemuidhinisha mgombea urais wa UDA William Ruto kuwania urais katika uchaguzi wa Agosti 9.

Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alitangaza hayo Jumamosi katika ukumbi wa Bomas of Kenya baada ya Ruto na mgombea mwenza wake Rigathi Gachagua kuwasilisha stakabadhi zinazohitajika.

"Ombi la William Ruto na mgombea mwenza kushiriki uchaguzi wa urais wa Agosti limeidhinishwa. Sasa nitawakabidhi cheti cha usajili," Chebukati alisema huku shangwe na nderemo kutoka kwa wafuasi wa Ruto na viongozi wa Kenya Kwanza walioandamana naye hadi Bomas zikishamiri hewani.

Naibu Rais William Ruto aliishukuru IEBC kwa jukumu lao la kuhakikisha Wakenya wanafanya uchaguzi wa kuaminika na kuwataka wawe waadilifu wanapotekeleza majukumu yao.

"Nimefurahi kupata cheti kitakachoniwezesha mimi na naibu wangu kushiriki katika uchaguzi wa Agosti. Mheshimiwa Mwenyekiti, tumejitolea kwa maadili tuliyotia saini... Tuna imani upo kwenye kazi na tutafanya kazi nanyi kwa bidii," alisema.

Kwa vyombo vya habari, DP alisema ni wakati wao kuwa waadilifu na wenye usawa wakati wa kuripoti kampeni za kisiasa kabla ya uchaguzi.

"Ni jambo la heshima zaidi kufanya. Tumeeleza wasiwasi huu. Pia tunawasihi (IEBC) muwahudumie wagombeaji wote katika kinyang'anyiro hiki kwa usawa," akasema.

"Tunaomba tu kutendewa haki... Tutashirikiana na Wakenya wote katika uchaguzi huu," alisema na kuwataka Wakenya kusalia na amani wakati wa kuandaa uchaguzi.

Baada ya kuwasilisha karatasi zake, Ruto ataingia jijini kuzuru mitaa mbalimbali jijini Nairobi kisha amalizie katika uwanja wa kihistoria wa Kamukunji lililo eneo bunge la Kamukunji.

Atakuwa akijipigia debe na vilevile kuwafanyia kampeni wagombeaji wake wa Kenya Kwanza wakati wa ziara yake.

Msafara wa Ruto utasimama angalau katika vituo saba ambapo atauza mtindo wake wa kiuchumi wa chini kwenda juu.

Ataanzia South C, South B, Mukuru, City Stadium, Gikomba, Majengo na hatimaye Kamukunji.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved