logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Huu sio wakati wa vurugu,'NCIC yawaonya wanasiasa huku ikilaani vikali ghasia za Jacaranda

Tume hiyo hata hivyo imesema kwamba imeanzisha uchunguzi,ili kuwakamata waliohusika

image
na Radio Jambo

Habari20 June 2022 - 12:47

Muhtasari


  • Tume hiyo hata hivyo imesema kwamba imeanzisha uchunguzi,ili kuwakamata waliohusika katika vurugu hivyo

Tume ya Kitaifa ya Uwiano na Utangamano (NCIC) imelaani vurugu viliyofanyika Jumapili tarehe 19 Juni 2022 katika uwanja wa Jacaranda jijini Nairobi.

Tume hiyo hata hivyo imesema kwamba imeanzisha uchunguzi,ili kuwakamata waliohusika katika vurugu hivyo.

"Kama Tume iliyopewa jukumu la kuwezesha kuishi pamoja kwa amani, tumezindua uchunguzi, na hivi karibuni tutawakamata wale waliohusika katika kuandaa na kutekeleza vurugu,"Ilisoma taarifa ya NCIC siku ya Jumatatu.

Aidha iliwaonya wanasiasa dhidi ya kutekeleza vurugu, huku ikisema kwamba huuu sio wakati wa vurugu kama nchi,inapoelekea katika uchaguzi mkuu wa Agosti.

"Kwa hili tunatoa taarifa kwa wanasiasa kwamba huu si wakati wa vurugu kama njia ya kufanya uhamasishaji wa kisiasa. Kama nchi na kama NCIC, tunasalia kujitolea kufikia maadili ya kisiasa katika uchaguzi mkuu wa 2022. Hatutavumilia majambazi ya kisiasa iliyoonyeshwa kwenye kiwanja cha Jacaranda jana. Kwa ajili hiyo, tunaviomba vyama vyote vya siasa sio tu kulaani vitendo hivyo Jacaranda, lakini pia kujitolea wenyewe, wanachama na wafuasi wao kwa siasa adabu katika kipindi hiki kigumu katika nchi yetu."

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved