logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Drama!Mwanamume akatiza mkutano wa Chebukati na wagombea Urais

Ruto aliwakilishwa na Gavana wa Turkana Josphat Nanok na katibu mkuu wa UDA Veronica Maina.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri29 June 2022 - 08:19

Muhtasari


  • Ruto aliwakilishwa na Gavana wa Turkana Josphat Nanok na katibu mkuu wa UDA Veronica Maina
  • Mgogoro wa wagombea wote ni upatikanaji wa mfumo shirikishi wa utambuzi wa wapiga kura

Mwanamume mmoja Jumatano alisababisha hali ya taharuki wakati wa mkutano kati ya wagombeaji urais na IEBC kuhusu kujitayarisha kwa wapiga kura.

Mtu huyo asiyejulikana alimwendea mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati na bango na kutoa matakwa wakati Chebukati alipokuwa akikaribia kuwaalika wagombeaji kueleza wasiwasi wao.

“Ninachotaka ni uhuru,” alisikika mtu huyo ambaye hakufahamika jina lake akipiga kelele huku watu wa taratibu wakimbeba bega juu kutoka nje ya chumba hicho.

IEBC kwa sasa inapokea maswala kutoka kwa wagombeaji urais yanayohusu michakato ya uchaguzi katika hoteli ya Windsor, Nairobi.

Mgogoro wa wagombea wote ni upatikanaji wa mfumo shirikishi wa utambuzi wa wapiga kura.

Isipokuwa William Ruto wa UDA ambaye hayupo kwenye mkutano huo, Raila Odinga wa Azimio, kiongozi wa Roots Party George Wajackoyah na David Mwaure Waihiga wa Agano wote wako pamoja na wagombea wenza wao.

Ruto aliwakilishwa na Gavana wa Turkana Josphat Nanok na katibu mkuu wa UDA Veronica Maina.

Mkutano huo ulitokana na nia ya tume kutotumia daftari la wapiga kura kwa mwongozo kuwatambua wapigakura siku ya uchaguzi endapo vifaa vya Kims vitashindwa.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved