logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pigo kwa Wanjigi baada ya Mahakama kuu kutupilia mbali kesi kuhusu kibali cha IEBC

Kulingana na Wanjigi, jinsi alivyofutiliwa mbali katika orodha ya mgombea urais ilitia shaka.

image
na Radio Jambo

Habari01 July 2022 - 09:49

Muhtasari


  • Kulingana na Wanjigi, jinsi alivyofutiliwa mbali katika orodha ya mgombea urais ilitia shaka
  • Kulingana na Wanjigi, Kamati ya Kusuluhisha Mizozo ya IEBC ilikosea kisheria kutupilia mbali malalamishi yake
Jimi Wanjigi

Mahakama Kuu imetupilia mbali ombi lililowasilishwa na mgombea urais wa Chama cha Safina Jimi Wanjigi akitaka jina lake lijumuishwe katika orodha ya wagombeaji urais katika Uchaguzi Mkuu wa Agosti 9.

Jaji Jairus Ngaah alitupilia mbali ombi hilo kwa msingi kwamba Wanjigi alikosa kuwasilisha kesi ya lazima mbele ya mahakama kuhusu ni kwa nini jina lake linastahili kupigwa kura.

Wanjigi aliwasilisha ombi hilo baada ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kukataa ombi lake la kuidhinishwa kuwania urais mwezi Agosti kwa kukosa shahada ya chuo kikuu. Alikuwa akiitaka mahakama kufutilia mbali uamuzi wa IEBC na kuamuru mwenyekiti Wafula Chebukati amteue kuwa mgombeaji urais.

Kulingana na Wanjigi, Kamati ya Kusuluhisha Mizozo ya IEBC ilikosea kisheria kutupilia mbali malalamishi yake.

"Agizo la Mandamus likimuelekeza Chebukati kujumuisha jina la Jimi Wanjigi kwenye karatasi za kura kwa uchaguzi wa urais uliopangwa kufanyika Agosti 9," ombi la Wanjigi linatafuta kwa sehemu.

Wanjigi amemkashifu Chebukati kwa kumnyima faida pakubwa yeye na kampeni yake baada ya kukosa kumwidhinisha kuwania  uchaguzi wa Agosti.

Kulingana na Wanjigi, jinsi alivyofutiliwa mbali katika orodha ya mgombea urais ilitia shaka.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved