logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nitafanya kazi yangu hadi dakika ya mwisho-Uhuru kwa wakosoaji wake

Uhuru alisema bado ana kazi nyingi anazofanya na hatakwenda hadi amalize zote.

image
na Radio Jambo

Makala12 July 2022 - 13:41

Muhtasari


  • Uhuru pia aliunga mkono mgombeaji urais wa Azimio Raila Odinga akisema ndiye mtu bora zaidi kumrithi

Rais Uhuru Kenyatta amemsuta naibu wake William Ruto kuhusu matamshi kwamba anafaa kuzingatia tu kustaafu kwake kabla ya uchaguzi wa Agosti 9, mwaka huu.

Uhuru ambaye alikuwa akizungumza jijini Nairobi alipozindua miradi alisema haendi popote hadi amalize kazi yake.

"Hawa wengine ni wa mdomo tu na matusi. Ukiwaona wanakutana wananizungumzia mimi," alisema.

"Sitafuti kura. Wananiambia nimalizie niende, wanataka niende wapi? Nitafanya kazi yangu hadi dakika ya mwisho."

Uhuru alisema bado ana kazi nyingi anazofanya na hatakwenda hadi amalize zote.

Uhuru pia aliunga mkono mgombeaji urais wa Azimio Raila Odinga akisema ndiye mtu bora zaidi kumrithi.

"Bado kuna kazi nyingi za mawazo. Hospitali zinafaa kufunguliwa.. Nitazifanya mpaka nimpe rais ajaye na naomba mtu ambaye nitampitishia rungu. Raila Odinga," alisema.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved