logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Siasa na masomo" Mbunge wa Kandara Alice Wahome avalia sare shuleni

"Masomo. Masomo. Masomo. Tumetimiza,” Mbunge wa Kandara Alice Wahome alisema.

image
na Radio Jambo

Burudani15 July 2022 - 05:25

Muhtasari


• Wiki chache zilizopita mbunge Oscar Sudi pia alionekana katika sare za shule

Mbunge wa kandara Alice Wahome

Mbunge wa Kandara mheshimiwa Alice Wahome ameingia katika chama cha wabunge na waheshimiwa walioonekana kwenye sare za shule katika kipindi hiki cha kampeni za kujipigia debe kuelekea uchaguzi mkuu wa Agosti 9.

Hii ni baada ya Wahome kutia nakshi kwenye sare maridadi ya shule mpya kabisa kwenye eneo bunge hilo, shule ya upili ya Waitua ambayo alikuwa akiifungua kuanza kuhudumia watoto kimasomo rasmi.

Katika rundo la picha alizozipakia kwenye ukurasa wake wa Facebook, Wahome alionekana akiwa miongoni mwa wanafunzi huku kweney video moja akionekana kukata utepe wa kuashiria kufunguliwa rasmi kwa mradi huo uliofadhiliwa na fedha za CDF ya eneo bunge la Kandara chini ya uongozi wake.

“Mwanafunzi nambari moja kwenye shule hii. Ikumbukwe shule ya upili ya Waitua ni miongoni mwa miradi tuliyoianzisha kutoka msingi mpaka kumalizika katika eneo bunge hili la Kandara. Masomo. Masomo. Masomo. Tumetimiza,” Mheshimiwac Wahome aliandika.

Huyu si mheshimiwa wa kuanza kuonekana akizundua miradi ya masomo kwenye shule huku akiwa katika sare za shule kwani wiki mbili zilizopita mbunge wa kapseret Oscar Sudi pia alionekana akiwa ndani ya sare ya shule moja katika eneo bunge lake wakati wa hafla.

Wabunge hawa wote wanaegemea mrengo wa naibu rais William Ruto na wote wanalenga kutetea nyadhifa zao kupitia chama cha UDA katika uchaguzi mkuu ujao wa Agosti 9.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved