logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Naibu Rais William Ruto ashiriki mdahalo wa urais

Wagombea wawili wa urais wameelezea kutoridhishwa kwao na kudokeza kwamba hawatahudhuria

image
na

Makala26 July 2022 - 13:14

Muhtasari


•Mdahalo huo unapeperushwa moja kwa moja kwenye vituo vyote vya TV na redio.

• Ruto aliwasili akiandamana na mkewe na iwafuasi wake.

Mdahalo wa Urais ambao umekuwa ukisubiriwa kwa hamu na gamu hatimaye umengóa nanga.

Mdahalo huo unapeperushwa moja kwa moja kwenye vituo vyote vya televisheni na redio kote nchini.

Naibu rais William Ruto anaendelea kueleza wakenya mambo ambayo analenga kuwafanyia.

Mgombea urais wa muungano wa Azimio One Kenya Raila Odinga alitarajiwa kushiriki mdahalo na Ruto lakini bado hawajawasili.

Awali mgombea urais wa Chama cha Roots George Wajackoyah alitaja kutotendewa haki akisema wagombeaji wote wanne wangepaswa kuwekwa pamoja kushiriki katika mdahalo huo pamoja.

Baada ya wandalizi kudinda kutimiza matakwa yake, Wajakoya alijiondoa kutoka mdahalo huo na kumuacha mgombea urais wa chama cha Agano David Waihiga Mwaure kujadili maswala yake pekee yake.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved