logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kakamega, Mombasa kufanya uchaguzi wa ugavana Agosti 23

Karatasi za kura za viti hivyo zilikuwa na picha na maelezo zisizo ya wagombeaji zisizo sawa.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri09 August 2022 - 15:10

Muhtasari


•Uchaguzi huo ulisitishwa pamoja na kura za wabunge huko Kacheliba na Pokot Kusini kutokana na mkanganyiko wa karatasi za kura.

•Kufikia mwisho wa upigaji kura saa kumi na moja jioni, Wanderi alisema Wakenya milioni 12,065,803 walinaswa kwenye KIEMS.

Mpiga kura akipiga kura katika kituo cha Shule ya Msingi ya Umoja. Upigaji kura ulianza vizuri katika sehemu nyingi za Nakuru

Uchaguzi wa ugavana Kakamega na Mombasa utafanyika Agosti 23.

Uchaguzi huo ulisitishwa pamoja na kura za wabunge huko Kacheliba na Pokot Kusini kutokana na mkanganyiko wa karatasi za kura.

Mnamo Jumatatu mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alisema karatasi za kura za viti hivyo zilikuwa na picha na maelezo zisizo ya wagombeaji zisizo sawa.

Jumanne jioni kamishna wa IEBC Francis Wanderi alisema kwamba uchaguzi huo pia utafanyika Kitui Rural na Rongai, kaunti ya Nakuru.

Hata hivyo, alisema wapiga kura katika eneo la Eldas wanapaswa kujiandaa kupiga kura Jumatano, Agosti 10 kuanzia saa kumi na mbili asubuhi.

Kufikia mwisho wa upigaji kura saa kumi na moja jioni, Wanderi alisema Wakenya milioni 12,065,803 walinaswa kwenye vifaa vya KIEMS kama walipiga kura.

Alisema idadi hiyo inawakilisha asilimia 56.17 ukiondoa wale waliotambuliwa kwa mikono.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved