logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamume akamatwa na panga,kisu katika kituo cha kupigia kura cha Homa Bay

Mmoja wa maafisa wa GSU alitilia shaka mshukiwa baada ya kuona kitu kimefichwa kiunoni mwake.

image

Uchaguzi09 August 2022 - 17:12

Muhtasari


  • Maafisa hao walimfunga pingu mshukiwa na kumwamuru alale chini, ambapo walimkuta akiwa na silaha hizo ghafi

Mwanamume mmoja alikamatwa Jumanne katika shule ya msingi ya Shauri Yako, kituo cha kupigia kura huko Homa bay, baada ya kupatikana na panga na kisu.

Katika video iliyosambaa mitandaoni, mwanamume huyo anaonekana akiwa amefungwa pingu na kuketi chini huku polisi wakimzunguka.

Alikamatwa wakati polisi walipokuwa wakisafisha kituo cha kupigia kura baada ya shughuli ya kupiga kura.

Mmoja wa maafisa wa GSU alitilia shaka mshukiwa baada ya kuona kitu kimefichwa kiunoni mwake.

Maafisa hao walimfunga pingu mshukiwa na kumwamuru alale chini, ambapo walimkuta akiwa na silaha hizo ghafi.

Alikabidhiwa kwa maafisa walio katika Kituo cha Polisi cha Homa Bay ambapo anazuiliwa kwa mahojiano zaidi.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved