logo

NOW ON AIR

Listen in Live

MC Jessy Akubali Kushindwa Ubunge South Imenti

"Binafsi nataka kumpongeza mshindani wangu anayestahili Dk Shadrack anapojitayarisha kuwa Mbunge mpya wa Imenti Kusini. Kwa wafuasi wangu jipeni moyo ni Siasa tu," - MC Jessy

image
na Davis Ojiambo

Uchaguzi10 August 2022 - 12:05

Muhtasari


  • • Jessy alikuwa anawania kama mgombea huru baada ya kunyimwa tikiti ya chama cha UDA
Mchekeshaji na mwanasiasa Jasper Muthomi almaarufu MC Jessy

Mchekeshaji Jasper Muthomi almaarufu MC Jessy amebwagwa katika uchaguzi wa ubunge Imenti ya Kusini na mshindani wake mkuu Dkt. Shadrack katika kinyang’anyiro hicho.

Jessy amejiunga na wanasiasa wengine wengi ambao wakeridhia matokeo hayo na amekubali kushindwa huku akimpongeza Dkt. Shadrack kwa ushindi huo huku akimtakia kila la kheri katika kuwafanyia wana Imenti Kusini kazi.

“Kwa Wananchi wa Eneo Bunge la Imenti Kusini, Ninawashukuru kwa Dhati kwa muda ambao tumetangamana wakati wa kampeni zetu. Imekuwa safari nzuri. Safari ya matukio ya ajabu ya kisiasa. Safari ya mioyo yenye ujasiri. Tutaendelea kushiriki tunapotarajia Wakati Ujao. Mungu akipenda. Binafsi nataka kumpongeza mshindani wangu anayestahili Dk Shadrack anapojitayarisha kuwa Mbunge mpya wa Imenti Kusini. Kwa wafuasi wangu jipeni moyo ni Siasa tu, tuendelee kusonga Imenti Kusini kama Jumuiya moja Kubwa,” Jasper Muthomi aliandika kwenye Instagram yake.

Awali kulikuwa na utata baada ya mchekeshaji huyo kusemekana kwamba amejitoa kwenye kinyang’anyiro ambapo alikuwa na nia ya kuwania kwa tikiti ya chama cha UDA ila baada ya tikiti hiyo kupewa kwa mshindani mwingine kweney kura za mchujo kwa jina Mwiti Kathaara.

Naibu rais William Ruto alikuwa ametangaza kwenye Twitter yake akisema kwamba Jessy angepokea kazi katika kamati ya kampeni zake ila muda mchache baadae alijitokeza wazi na kupinga madai hayo huku akisema kwamba atakuwa debeni kama mgombea huru.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved