logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Waiguru alalamikia wizi wa kura huku hesabu za kura zikiendelea Kirinyaga

Ngirici alieleza imani yake katika mchakato wa uchaguzi.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri10 August 2022 - 15:37

Muhtasari


•Waiguru alidai kuwa masanduku mawili ya kura yaliingizwa katika kituo cha kuhesabia kura cha Kianyaga.

Gavana wa Kirinyaga Ann Waiguru akipiga kura katika shule ya msingi ya Kiamugumo, kaunti ya Kirinyaga.

Gavana wa Kirinyaga Ann Waiguru ameibua madai ya wizi wa kura huku ujumuishaji wa kura ukiendelea.

Alidai kuwa masanduku mawili ya kura yaliingizwa katika kituo cha kuhesabia kura cha Kianyaga.

"Wizi wa kura mchana peupe -Sanduku mbili za kura zilizo na karatasi za magavana zimeingizwa Kianyaga kupitia mlango wa nyuma mchana kweupe!"

"Lazima ziondolewe na kuhesabiwa kwa kura lazima kusimamishwe," Waiguru aliongeza.

Gavana huyo anatafuta kutetea kiti chake kwa muhula wa pili kutumia tiketi ya Chama cha United Democratic Alliance (UDA).

Mpinzani wake mkuu, Wangui Ngirici ni mgombea huru.

Siku ya Jumanne, Ngirici alieleza imani yake katika mchakato wa uchaguzi.

Akizungumza katika kituo cha kupigia kura cha Kaitheri Polytechnic, mjini Kerugoya muda mfupi baada ya kupiga kura, mgombeaji huyo wa kujitegemea alliwataka wafuasi wake kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kuleta mabadiliko.

Alitaja zoezi hilo kuwa la kuleta mabadiliko na kuwataka wapiga kura kutekeleza wajibu wao wa kiraia kwa busara.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved