logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mohammed Ali ahifadhi kiti cha Mbunge wa Nyali

Ali alipata kura 32,988 dhidi ya mpinzani wake mkuu Said Abdalla almaarufu Saido wa ODM

image
na Radio Jambo

Habari11 August 2022 - 18:41

Muhtasari


  • Ali alipata kura 32,988 dhidi ya mpinzani wake mkuu Said Abdalla almaarufu Saido wa ODM aliyepata 18,642
Mohammed Ali

Mbunge wa Nyali Mohammed Ali amehifadhi kiti chake katika uchaguzi mkuu uliokamilika hivi punde.

Ali alipata kura 32,988 dhidi ya mpinzani wake mkuu Said Abdalla almaarufu Saido wa ODM aliyepata 18,642.

Matokeo hayo yalitangazwa na afisa mrejeshaji kura katika eneo bunge la Nyali John ole Taiswa katika kituo cha kujumlisha kura za eneo bunge hilo, Mamlaka ya Kitaifa ya Mafunzo ya Viwanda (Nita) Mombasa.

Wapinzani wanne walikuwa wanawania kiti hicho cha mbunge wa nyali katika uchaguzi mkuu..

Moha aliwashukuru wafuasi wake katika hotuba yake ya kukubalika akiwaahidi kuwa atafanya kile alichoahidi wakati wa kampeni.

“Nataka kuwashukuru kwa kunichagua, wale tulikua tunashindana nao sasa ni wakati wa kuchapa kazi pamoja,” alisema.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved