logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Otiende Amollo achaguliwa tena kuwa mbunge wa Rarieda

Ushindi wa Amollo unaashiria mwanzo wa muhula wake wa pili kama mbunge wa Rarieda.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri11 August 2022 - 01:09

Muhtasari


•Mbunge huyo alihifadhi kiti chake baada ya kupata kura 37,676 dhidi ya mpinzani wake wa karibu Agustin Adhola aliyepata 23,266 chini ya chama cha United Democratic Movement (UDM).

Mbunge wa Rarieda Otiende Amollo

Mbunge wa Rarieda Otiende Amollo amehifadhi kiti chake.

Ushindi wa Amollo unaashiria mwanzo wa muhula wake wa pili kama mbunge wa Rarieda.

Mbunge huyo alihifadhi kiti chake baada ya kupata kura 37,676 dhidi ya mpinzani wake wa karibu Agustin Adhola aliyepata 23,266 chini ya chama cha United Democratic Movement (UDM).

Amollo alikuwa akigombea kutumia tikiti ya Orange Democratic Party (ODM).

Wakili huyo wa mahakama kuu alikabidhiwa uteuzi wa moja kwa moja na chama cha ODM kwa sababu hakuwa na mshindani.

Alichaguliwa kwa mara ya kwanza kama mbunge wa eneo bunge la Rarieda katika uchaguzi mkuu wa 2017.Amollo alihudumu kama Ombudsman katika Tume ya haki ya utawala kwa miaka miwili kuanzia 2014 hadi 2016.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved