logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Igathe akubali matokeo na kumhongera Sakaja kwa ushindi

“Ninakubali uamuzi wa watu wa Nairobi na kuwashukuru wafuasi wetu wote. Gavana wa Nairobi ni Mheshimiwa Johnson Sakaja. Hongera! Mungu ibariki Kenya,” Polycarp Igathe aliandika.

image
na Radio Jambo

Habari14 August 2022 - 07:08

Muhtasari


• Msimamizi wa uchaguzi katika kaunti ya Nairobi, Albert Gogo alimtangaza Sakaja aliyekuwa akiwania kwa chama cha UDA kuwa mshindi

Aliyekuwa mgombea wa ugavana Nairobi, Polycarp Igathe

Aliyekuwa mgombea ugavana Nairobi Polycarp Igathe amenywea na kukubali matokeo ya uchaguzi baada ya mshindani wake Johnson Sakaja kutangazwa kuwa mshindi wa kiti hicho na kuwa rais wa kaunti hiyo ambayo ni kitovu cha uchumi wa taifa la Kenya.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Igathe amempongeza Sakaja kwa ushindi huo mkubwa na kumtakia kila la kheri katika safari yake ya kuwatumikia wana Nairobi.

“Ninakubali uamuzi wa watu wa Nairobi na kuwashukuru wafuasi wetu wote. Gavana wa Nairobi ni Mheshimiwa Johnson Sakaja. Hongera! Mungu ibariki Kenya,” Polycarp Igathe aliandika.

Msimamizi wa uchaguzi katika kaunti ya Nairobi, Albert Gogo alimtangaza Sakaja aliyekuwa akiwania kwa chama cha UDA kuwa mshindi baada ya kupata kura zaidi ya laki sita huku Igathe akiibuka wa pili kwa kura zaidi ya laki tano.

Igathe sasa anajiunga katika orodha ya wanasiasa wengi ambao wamekubali matokeo bila ya kutaka kuyapinga mahakamani kama ambavyo imekuwa ikishuhudiwa katika chaguzi za awali.

Sakaja alimshinda kwa zaidi ya kura laki moja na hili linatajwa kuwa pigo kubwa kwa muungano wa Azimio la Umoja One Kenya waliokuwa wakitaka kuwa na udhibiti wa jiji la Nairobi katika nyadhifa za juu zote ila Sakaja akavuruga mipango yao.

Igathe sasa anajiunga na Moses Kuria aliyekuwa akiwania ugavana Kiambu kukubali matokeo katika nyadhifa hiyo ya juu katika serikali za ugatuzi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved