logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tuna imani kuwa tutashinda uchaguzi, Wajackoyah asema

Wajackoyah alisema atahutubia taifa baada ya rais kutangazwa.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri14 August 2022 - 17:24

Muhtasari


  • Hata hivyo, Mwaure alikubali kushindwa na kumuunga  mgombea urais wa UDA William Ruto
Mgombea urais kutoka chama cha Roots, wakili msomi George Wajackoyah

Mgombea urais wa chama cha Roots George Wajackoyah amesema wana imani kwamba watashinda uchaguzi ambao umekamilika hivi punde.

Kupitia taarifa, Wajackoyah alisema ikiwa mchakato huo ni wa haki, huru na wa kuaminika, watajinyakulia mamlaka.

“Kama mnavyofahamu, mgombea wetu wa urais ni mmoja kati ya Wakenya wanne wanaosaka afisi ya juu zaidi nchini ili kubadilisha nchi yetu na kuifanya Kenya kuwa gwiji la mwanauchumi,” ilisoma sehemu ya taarifa hiyo.

Wajackoyah alisema atahutubia taifa baada ya rais kutangazwa.

"Wananchi walitekeleza awamu ya kwanza, na awamu ya pili na IEBC, chombo hicho kikatiba kiliidhinisha kujumlisha kura na kumtangaza mshindi. Mgombea wetu atahutubia taifa baada ya kutangazwa rasmi na IEBC," akasema.

Kinyang'anyiro cha urais kilikuwa kimewavutia wagombeaji wanne; Kiongozi wa chama cha UDA William Ruto, Raila Odinga wa Azimio, na kiongozi wa chama cha Agano Waihiga Mwaure.

Hata hivyo, Mwaure alikubali kushindwa na kumuunga  mgombea urais wa UDA William Ruto.

Mwaure alisema ameona takwimu zilizoonyeshwa na IEBC zinamuunga mkono Ruto na alikuwa anakubaliana na manifesto ya UDA.

"Baada ya mazungumzo ya kina na timu zetu huko Bomas, tumekuwa tukifuata utaratibu unaoendelea na kuashiria kuwa takwimu ziko na bila shaka zimekuwa zikimuunga mkono William Ruto," alisema.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved