Idadi ndogo ya wapiga kura yashuhudiwa Mombasa huku uchaguzi wa gavana ukifanyika

Kaunti hiyo ambayo ina wapigakura zaidi ya 600,000 waliojiandikisha, inakumbwa na idadi ndogo ya wapiga kura.

Muhtasari

•Vituo vingi vya kupigia kura vilifunguliwa kwa wakati, saa kumi na mbili asubuhi.

•Kinyang'anyiro cha ugavana kimevutia wagombeaji saba. 

Waliojitokeza kwa wingi katika shule ya msingi Mikindani yenye vituo 9 vyenye jumla ya wapiga kura 5624 waliojiandikisha.
Waliojitokeza kwa wingi katika shule ya msingi Mikindani yenye vituo 9 vyenye jumla ya wapiga kura 5624 waliojiandikisha.
Image: STEVE MOKAYA

Zoezi la kumpigia kura gavana ajaye wa Mombasa limeanza katika vituo vingi vya kupigia kura ndani ya kaunti ya Mombasa.

Vituo vingi vya kupigia kura vilifunguliwa kwa wakati, saa kumi na mbili asubuhi.

Kinyang'anyiro cha ugavana kimevutia wagombeaji saba. Abdulswamad Nassir wa ODM na Hassan Omar wa UDA ndio farasi wakuu katika kinyang’anyiro hicho.

Hata hivyo, kaunti hiyo ambalo ina zaidi ya wapiga kura 600,000 waliojiandikisha, linakabiliwa na idadi ndogo ya wapigakura wanaojitokeza kupiga kura.

Katika Eneo bunge la Nyali, ambalo lina vituo 195 vya kupigia kura na zaidi ya wapiga kura 124,000 waliojiandikisha, vituo vya kupigia kura vilibakia bila watu.

Shule ya Msingi ya Maweni, ambayo ina wapigakura zaidi ya 5,000 waliojiandikisha, na Shule ya Msingi wa Ziwa La Ng’ombe ambayo ina wapigakura zaidi ya 7,000 waliojiandikisha vilikuwa na wapigakura wachache sana waliojitokeza kupiga kura kufikia saa moja asubuhi Jumatatu.

Shule ya Msingi ya Tumaini, pia ndani ya eneo bunge la Nyali, inakumbwa na idadi ndogo ya wapiga kura.

Vile vile hali kama hiyo imeripotiwa katika maeneo bunge matano yaliyosalia ya Kisauni, Mvita, Likoni, Jomvu, na Changamwe.

Nassir anatarajiwa kupiga kura yake katika Shule ya Msingi ya Mvita mwendo wa saa tisa asubuhi, Omar atapiga kura yake katika Zahanati ya Kandherboy ndani ya Mvita pia.

Gavana anayemaliza muda wake Hassan Joho atapiga kura katika Uwanja wa Mbuzi huko Nyali