logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilipogundua mume wangu ananidanganya,nilimdanganya na wanaume 3-Muigizaji Njambi

Njambi alisema kwamba aligundua mumewe anadanganya, hii ni baada ya kuenda kwa wiki mzima akirudi anamwambia kwamba ametoka baa

image
na Radio Jambo

Habari22 March 2021 - 10:46

Muhtasari


  • Studioni katia kipindi cha ilikuaje tulikuwa na muigizaji Njambi ambaye alizungumzia vurugu vya nyumbani ambavyo alipitia katika ndoa yake ya awali

Studioni katia kipindi cha ilikuaje tulikuwa na muigizaji Njambi ambaye alizungumzia vurugu vya nyumbani ambavyo alipitia katika ndoa yake ya awali.

Njambi alisema kwamba aligundua mumewe anadanganya, hii ni baada ya kuenda kwa wiki mzima akirudi anamwambia kwamba ametoka baa, ilhali hakuwa anapokea simu zake.

"Mume wangu alikuwa anatoka kwa nyumba kwa wiki mzima, nikimpigia simu hapokei, akirudi nyumbani ananiambia kwamba ametoka baa

 

Niligundua kwamba anatoka nje ya ndoa, na mimi nikaamua kumdanganya na wanaume watatu, pia alijua kwamba natoka nje ya ndoa, siku moja alirudi nyumbani na kuniuliza kama hamna kiberiti nilimwambia kwamba iko jikoni

hapo nilitoroka, nilienda kujificha chini ya gari, alinichapa lakini niliokolewa na majirani,niliporudi kwetu baba yangu aliniambia asiwahi sikia kwamba nimerudi kwa huyo mwanamume," Alizungumza NJambi.

Njambi aliwahimiza wakenya wapendane licha ya changamoto ambazo wanapitia.

Muigizaji huyo pia alifichua kwamba alipokuwa chuo kikuu aliwachumbia 'sponsor' si kwa ajili wazazi wake hawanempa pesa bali kwa ajili ya shinikizo kutoka kwa marafiki.

Kwa mengi zaidi tembelea Radiojambo youtube.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved