logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: Mama ajuta kumtusi mwanawe wa miaka 19 kwa kuhama nyumbani, kutomlipia dadake karo

Sam alipopigiwa simu, mama yake alichukua fursa hiyo kumuomba msamaha ila akakata simu kabla hawajazungumza.

image
na SAMUEL MAINA

Vipindi19 February 2024 - 06:18

Muhtasari


  • •Bi Maggy alisema uhusiano wake na mwanawe uliharibika baada ya yeye kumtaka kijana huyo mwenye umri wa miaka 19 amlipie karo dadake mdogo.
  • •Sam alipopigiwa simu, mama yake alichukua fursa hiyo kumuomba msamaha ila akakata simu kabla hawajazungumza.
GHOST NA GIDI STUDIONI

Katika kitengo cha Patanisho, mwanamke aliyejitambulisha kama Maggy Lenduda (33) kutoka Samburu alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na mwanawe Sam Lenduda ambaye alikosana naye mwishoni mwa mwaka jana.

Bi Maggy alisema uhusiano wake na mwanawe uliharibika Desemba mwaka jana baada ya yeye kumtaka kijana huyo mwenye umri wa miaka 19 amlipie karo dadake mdogo, jambo ambalo hangeweza kwani hakuwa na kazi.

Alisema alimkasirikia sana mwanawe hadi kumtumia ujumbe mbaya ambao uliharibu uhusiano wao.

"Kijana yangu alimaliza shule akasaka kibarua. Nikamwambia asisahau sisi tulio nyumbani, nikamwambia wakati akipata kibarua atukumbuke sisi nyumbani," Maggy alisimulia.

Aliongeza, "Alienda Nairobi na kukatiza mawasiliano. Kuna kijana alitoka Nairobi akaja nyumbani na akaniambia kijana wangu bado hajapata kazi, nikamtumia meseji mbaya. Nilimuuliza mbona alienda Nairobi na hakuna mawasiliano. Sikujua kwamba hakuwa amepata kazi."

Sam alipopigiwa simu, mama yake alichukua fursa hiyo kumuomba msamaha ila akakata simu kabla hawajazungumza.

Bi Maggy alisema, "Nikijaribu kumpigia anasema yuko bize. Wakati mwingine nikimpigia anakata simu. Mimi sina bwana, ni mtu najitegemea. Aliondoka tu hivyo akatuacha nyumbani.

Sikutusi yeye, nilimuuliza ameondoka akaanza kujishughulikia. Labda ameenda akapata boma na msichana akaanza kushughulikia yeye na kutusahau."

Alipopewa fursa ya kumuomba mwanawe msamaha hewani, Maggy alisema, "Mimi bado ni mama yake na hakuna mahali atapata mwingine. Akumbuke tu mahali tumetoka, ajaribu kukumbuka maisha ya nyumbani. Naomba awe huru kwangu na mimi niwe huru kwake ili tuweze kusaidiana maishani."

Je, maoni yako ni yepi kuhusu Patanisho ya leo?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved