logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kuwa mzazi kumenibadili sana katika maisha yangu-Muigizaji Nick Mutuma

Nimekuwa na Bridget Shighadi kwa miaka kumi, kuna wakati nilimezea mwanamke mwingine mate

image
na Radio Jambo

Habari16 February 2021 - 10:50

Muhtasari


  • Nick Mutuma aeleza jinsi kuwa mzazi kumebadili maisha yake huku akisema kwamba kulea ni kazi ngumu

Leo katika kitengo cha ilikuaje tulikuwa naye muigizaji Nick Mutuma ambaye alifunguka kuhusu maisha yake.

"Nilianza kazi ya uigizaji mwaka wa 2008, ambapo niliigiza kama mwanamume mbaye anapenda 'sugarmummies' wazazi wangu walishangaa sana lakini niliwaeleza

Nimekuwa na Bridget Shighadi kwa miaka kumi, kuna wakati nilimezea mwanamke mwingine mate lakini ni kawaida ya wanaume kusifu urembo wa mwanamke mwingine," Alisema Mutuma.

 

Alipoulizwa kwanini mara kwa mara huwa hawapakii picha zao pamoja Nick alikuwa na haya ya kusema.

"Tunapenda maisha yetu yawe ya siri kando na uigizaji, Bridget si mwanamke ambaye anapenda kiki wala kuweka maisha yake hadharani

kuwa mzazi kumenibadilisha sana, kwa maana nimeacha kuzurura kila mara, kulea si jambo rahisi kwa hakika

Mahali tumefika kama wapenzi wawili katika sekta ya uigizaji kuna uigizaji mwingine hatuwezi fanya,"


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved