logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila ndiye sababu yangu ya kufahamika namshukuru-Shebesh

Nataka kuwashauri wanasiasa ambao wanatoka katika vyama vya siasa wanapaswa kutoka kwa heshima

image
na Radio Jambo

Habari08 July 2021 - 10:54

Muhtasari


  • Shebesh aweka wazi kwamba Raila ndiye alifanya afahamike kwenye sekta ya siasa

Katika kitengo cha ilikuaje tulikuwa naye Katibu mwandamizi wa huduma kwa umma Rachel Shebesh ambaye alihitimu miaka 50 wikendi iliyopita.

Huku akizungumzia safari yake ya siasa Shebesh aliweka wazi kuwa anamshukuru Raila kwa maana ndiye alifanya afahamike haswa katika sekta ya kisiasa.

"Raila Odinga ndiye sababu yangu ya kufahamika sana katika siasa, kama sio yeye singekuwa mahali nilipo na namshukuru sana

Nataka kuwashauri wanasiasa ambao wanatoka katika vyama vya siasa wanapaswa kutoka kwa heshima, nilipotoka katika chama cha ODM nilitoka na heshima,"

Pia mwanasiasa huyo alikuwa mwakilishi wa wanawake wa kwanza katika kaunti ya Nairobi, na akizungumzia kazi yake ambayo huwa anajivunia nayo alipokuwa kwenye usukani alikuwa na haya ya kusema.

"KIle kitu najivunia ni vile niliweza kuwasaidia watu walemavu na watoto walemavu,na wakati Esher Passaris alishinda mwaka wa 2017, nilimwambia aendeleze kazi ambayo nilikuwa nimeanzisha na ameweza kufanya hayo

Siwezi kumlaumu mtu yeyote kwa kupoteza, kiti mwaka wa 2017,sianamengi ya kujihusisha nayo katika uchaguzi mkuu ujao nataka tu kuwatumikia wananchi,"Shebesh alizungumza.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved