logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sijawahi muona baba yangu,nilimuona siku ya mazishi yake-Rich Mavoko afichua

Kuna kipindi ambacho Mavoko alikuwa, kwenye lebo ya muziki ya Wasafi

image
na Radio Jambo

Burudani16 July 2021 - 10:16

Muhtasari


  • Rich Mavoko afichua haya kuhusu maisha yake ya utotoni

Katika kitengo cha ilikuaje tulikuwa naye msanii kutoka Tanzania Rich Mavoko. ambaye amekuja Kenya kuzindua albamu yake.

Kuna kipindi ambacho Mavoko alikuwa, kwenye lebo ya muziki ya Wasafi, msanii huyo aliweka wazi kuwa kabla ya kujiunga na WCB alikuwa anaimba.

"Nilikuwa ninaimba kabla ya Wasafi. Mimi sikutafuta Wasafi. Nilianza kuimba baada ya kumaliza kidato cha 4. Nina watoto 2, mama tofauti waliniachia watoto na wao wakaendelea na maisha yao

Mimi ni mtoto wa 5, kitinda minda. Sisi tumelelewa na mama tu. Sijawahi kumuona babangu ila tulikuwa tunazungumza. nilimuona siku ya mazishi yake," Aliongea Mavoko.

Huku akizungumzia usanii wake msnii huyo alisema,

"Nina maono makubwa sana na maono yangu yanategemea support ya mashabiki wangu. Nitatoa albamu yangu mwaka huu.."

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved