logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanavlogu Kelvin Kinuthia azungumza kuhusu suala la jinsia yake

Alisema kuwa jeni za familia yake na lishe bora zimechangia sana katika unene wa makalio na kiuno chake.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri02 March 2022 - 11:12

Muhtasari


  • Kinuthia alisema kuwa jeni za familia yake na lishe bora zimechangia sana katika unene wa makalio na kiuno chake
Kelvin Kinuthia katika studio za Radio Jambo

Mwanavlogu Kelvin Kinuthia amepatia watu uhuru wa kumtambulisha kama mwanaume ama mwanamke.

Akizungumza na Massawe Japanni katika kipindi cha Bustani la Massawe, Kinuthia alisema hana tatizo lolote kutambulishwa na jinsia yoyote ile.

"Ningependa kuitwa Kinuthia tu, hiyo ni sawa. Mi husema kile mtu atataka kuniita,ni sawa. Mimi niko sawa. Ukiniita mwanamke siweze kuhukumu kwa sababu hata navalia kama mwanamke," Alisema.

Mwavlogu huyo hata hivyo alikataa kuweka wazi jinsia yake halisi ambayo imeendelea kuibua utata mwingi miongoni mwa watumizi wa mitandao ya kijamii.

Kinuthia alisema kuwa jeni za familia yake na lishe bora zimechangia sana katika unene wa makalio na kiuno chake.

"Sijawahi enda kuangaliwa mbona nimeumbwa hivi. Lakini nadhani ni kitu iko kwa familia. Ata mama ako hivi tu. Pia ni kulula vizuri, kuleni vizuri," Alisema.

Alisema kuwa atazungumzia suala la jinsia yake halisi kikamilifu wakati atajihisi kuwa tayari.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved