logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanadada alalamika kuhusu mumewe kuvaa nguo zake za ndani

Mwanadada amefunguka kwamba bwana yake alikuwa anachukua nguo zake na kuvalia mpaka zile zinazovaliwa na ndani.

image
na Japheth Nyongesa

Mahojiano10 March 2025 - 14:50

Muhtasari


  •  Mwanaume huyo hakuwa anavalia tu nguo za ndani pekee lakini hata suruali zake ambazo amezinunua yeye mwenyewe mume wake alikua anachukua na kutembea nazo hadharani.
  • Mwanamke huyo pia alifichua kweamba baada ya kushindwa kununua mavazi yake mwenyewe na kuanaza kuvalia nguo za mkewe bado aliendelea kumutesa na kumpiga kila wakati bila kukoma.

Chupi

Mwanadada amefunguka na kueleza kwamba bwana yake alikuwa anachukua nguo zake mara kwa mara na kuvalia mpaka zile za  ndani.

Mwanamke huyo kwenye mahojiano na mtangazaji wa Radio Jambo Massawe Japani alieleza kwamba alikuwa anaudhika sana na tabia za mumewe kuchukua nguo zake na kwenda kucheza nazo kucheza mpira mbele ya watu na hata wakati mwingine kutembea nazo hadharani.

"Unaona hizi baika za mademu, hizi zenye hazina lens, na alikuwa mchezaji wa mpira, hizo ndizo alikuwa anachukua anavaa sasa ndio anasimama nazo kwa goli... Ile sasa amesharudi kwa nyumba ndio nashindwa bro kumbe ulienda na hii ananiambia hii ndo nilitumia kama short ya ball," alifuchua mwanadada huyo.

Aliendelea na kueleza kwamba mwanaume huyo hakuwa anavalia tu nguo za ndani pekee lakini hata suruali zake ambazo amezinunua yeye mwenyewe mume wake alikua anachukua na kutembea nazo hadharani.

"Sasa ikakuja ni surualli ya jeans, alikuwa anavaa hipster zangu. Yaani bro akitoka ameng'ara kumbe ameng'aria nguo yangu ya demu,' alieleza zaidi.

Mwanamke huyo pia alifichua kwamba baada ya kushindwa kununua mavazi yake mwenyewe na kuanza kuvalia nguo za mkewe bado aliendelea kumutesa na kumpiga kila wakati bila kukoma.

"Bro alikuwa anachapana, unasikianga kiboko. Hakununulia panti, hawezi ata kujinunulia nguo, hawezi kujinunulia boxer lakini bado anakutandika. Ashindwe popote alipo ata sai. Skini tites zangu za black alikuwa anakata inakuwa kama shoti na anavalia," aliweka wazi mwanadada huyo.

Aliendelea mbele na kueleza kwamba mwanaume huyo alikuwa kati ya yumri wa miaka 24 na 25 kwni alikuwa anamzidi na miaka kama mitatu. "Alikuwa kati ya miaka 24 na 25 maana mimi nilikuwa karibu 22" alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved