logo

NOW ON AIR

Listen in Live

PATANISHO:Mke wangu aliniacha baada ya kugundua ndugu yangu mdogo amekuwa akimtumia pesa

Baada ya kufanya juhudi zetu za kumpigia mkewe Nancy simu alikuwa na haya

image
na Radio Jambo

Burudani23 November 2020 - 05:48

Muhtasari


  • Ni kama nilikuwa  kijakazi wake na mlinzi wake kwa maana sijapata chochote katika ndoa hii wacha tu mtoto
  • Mke wangu alienda baada ya yangu kumuuliza kwanini amekuwa akitumiwa pesa na ndugu yangu mdogo

Leo katika kitengo cha patanisho bwana Masinde alituma ujumbe apatanishwe na mkewe ambaye wamekuwa kwa ndoa kwa miaka mitano na walikosana wiki jana baada ya kugundua mkewe amekuwa akitumiwa na ndugu yake mdogo.

"Wiki jana nilikuwa na simu ya mke wangu , kuangalia simu yake amekuwa wakizungumza na ndugu yangu mdogo na kuwa amekuwa akimtumia pesa nilipomuuliza alikasirika na kuenda kwao

Tumebarikiwa na mtoto mmoja." Alieleza Masinde.

Baada ya kufanya juhudi zetu za kumpigia mkewe Nancy simu alikuwa na haya ya kusema;

"Sitaki mambo ya huyu mwanamume, kwani bibi ambao alikuwa anawaleta nyumbani amewakataa, ndugu yake alikuwa ananitumia pesa ya matanga na wala hajawahi nitumia pesa

Kila mwaka maisha ni yale yale, kukosana kila wakati ni kisirani aliniambia kwamba mimi ni bibi wa familia

Mimi ni malaya aoe watu watakatifu kwa maana mimi si mtakatifu, ni kama nilikuwa mlinzi wake kwa maana amekuwa akikuja nyumbani saa sita ya usiku

Mimi nikama nilikuwa kijakazi wake, mimi simtaki nimempea ruhusa aweze kuoa na mimi nitatafuta mwanamume wa kuoa kama ni mtoto ambaye unataka kuja umchukue."

Kwa mengi zaidi tembelea radiojambo youtube.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved