logo

NOW ON AIR

Listen in Live

PATANISHO:Nilikosana na mke wangu baada ya mimi kwenda nje ya ndoa

Aliambiwa na marafiki zangu ambao waliniona naye, tumebarikiwa na watoto watatu

image
na Radio Jambo

Habari01 December 2020 - 05:46

Muhtasari


  • Nilipata mpango wa kando kaunti zilipofungwa kwa ajili ya kuthibiti kusambaa kwa virusi vya corona
  • Mkewe Julius alisema kwamba imekuwa ni mazoea kwa mumewe kukuwa na mipango wa kando

Bwana Julius,30, alituma ujumbe ili apatanishwe na mkewe ambaye wamekuwa katika ndoa kwa miaka kumi.

"Wakati nchi na kaunti zilikuwa zimefungwa kwa ajili ya kuthibiti kusambaa kwa corona, nilipata mpango wa kando baada ya kufunguliwa mke wangu alifahamu kuwa nilikuwa na mpango wa kando

Aliambiwa na marafiki zangu ambao waliniona naye, tumebarikiwa na watoto watatu." Alisema JUlius.

 
 

Baada ya kufanya juhudi zetu za kumpigia mkewe Elizabeth alisema kwamba imekuwa mazoea ya mumewe kufanya hayo na kuenda nje ya ndoa;

"Mimi nilimsamehe  kitambo, lakini imekuwa mazoea kwa maana amekuwa akifanya hayo nikijua mpango wake wa kando anamuacha na kuenda anatafuta mwingine huku akiniambia ya kwamba atabadilika lakini habadiliki

Mume wangu aliniambia nikae mashambani aende kazi kumbe yeye anaenda kutafuta wanawake wengine." Alisema Elizabeth.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved