- William alisema kwamba mkewe huwa anaenda nje akienda kazi usiku
- Mkewe naye alisema kwamba mumewe hajakuwa akijukumikia mahitaji ya nyumbani huku ikimlazimu kutafuta kazi
Bwana William Rono alituma ujumbe apatanishwe na mkewe ambaye alidai alikuwa anaenda nje ya ndoa.
"Nimekuwa nikienda kazi usiku, nikirudi nyumbani nampata mke wangu hayuko, nimefanya uchunguzi na kujua kuwa nikitoka usiku nikienda kazini anatoka anaenda." Rono Alieleza.
Baada ya mkewe Faith kuzungumza kuhusu madai hayo alikuwa na haya ya kusema,
"Rono hajakuwa akijukumika nyumbani, hata hajui watoto wanakula nini au penseli ni pesa ngapi
Ni mimi nimekuwa nikitoka nje na kutafuta kazi ili watoto wangu wawezze kula na kutimiza mahitaji yao
Nikipigiwa simu lazima aangalie ni nani anachukua namba ya simu anamtumia mama yangu,endapo nimemuitisha pesa ya kununua bidhaa za nyumbani huwa ananitetesha
Tangu watoto waende nyumbani hajwahi tuma hata shillingi moja hajui watoto wanakula nini, ndio alinioa nikiwa na mtoto mmoja na tukabarikiwa na wengine wawili
Nimechoka sasa staki mambo yake." Faith Aliongea.