- Mke wangu aliniacha baada yangu kuongea na mwanamke mwingine
- Simiyu alisema kwamba mkewe ana ujauzito wake na wamekuwa kwa ndoa kwa zaidi ya mwaka mmoja
Bwana Alex Simiyu alituma ujumbe apatanishwe na mke wake ambaye walikosana wiki jana baada ya kuongea na mwanamke mwingine.
Simiyu alisema kwamba mkewe ana ujauzito wake na wamekuwa kwa ndoa kwa zaidi ya mwaka mmoja.
"Nilikosana na mke wangu baada yangu kuongea na mwanamke ambaye tunafanya kazi naye, nilipoitisha namba yake mke wangu alijifanya amelala
nilipompigia mwanamke huyo alinyanyuka na kukasirika kisha akaenda,amekuwa akinishuku kuwa nina wanawake wengine nje," Alieleza Simiyu.
Baada ya kutafuta mkewe Rose alikuwa na haya ya kusema.
"Mwanamume huyo amenipitishia mambo mengi sana, mimi nilimsamehe licha yake kunioa hajawahi nipeleka kwa wazazi wake sijui ni mume wangu au ni nini
Sasa hivi nina ujauzito wa miezi nane, hajanunua kitu chochote cha mtoto ata suruali ya shillingi kumi
Hajui ukitaka ng'ombe itoke maziwa lazima ilishwe mzuri, kwa hivyo anapaswa kutoboka pesa, nataka afanye yote ambayo tulikubaliana na abadilike nitarudi,"
Kwa uhondo zaidi tembelea Radiojambo youtube.