PATANISHO:Nilimpata mume wangu 'lodging' mara nyingi

Muhtasari
  • Niliachana na mke wangu baada yangu kuenda kutafuta kazi na kumuacha
Gidi na Ghost

Bwana Geoffrey alituma ujumbe il apatanishwe na mke wake Serah ambaye amekuwa kwa ndoa naye kwa miaka 11.

Geoffrey alisema kwamba alienda kazi ghafla bila kumwambia mkewe, na tangu siku hiyo hapokei simu zake.

"Naomba mnipatanishe na mke wangu wa miaka 10. Nilienda kazi ghafla bila kumuelezea na tangu siku hiyo hapokei simu zangu

 

Sijawahi kurudi nyumbani tangu nipate hiyo kazi. Hata nilipata ajali nikalazwa kwa wiki 2, hakujibu hata jumbe zangu

Niliuza ng'ombe ili niende kazi," Alieleza Geoffrey.

Baada ya kufanya juhudi za kumpigia mkewe simu, Serah aliapa kutorudiana na mumewe, huku akisema amempata kwenye vyumba vya kulala na wanawake mara nyingi.

"Sitawahi kumsamehea milele na milele kwa yale amenitendea kwa miaka 11 ya ndoa. Mipango ya kando anayo mingi, anatusi hadi wazazi wangu

Kabla atoroke aliuza ndume na hakuacha hata shilingi 50. Nimemfumania mpaka 'lodging' na wanawake

tulifungiwa nyumba na nakahama sasa ndio anakuja kusema kwamba anataka kunitumia pesa, huyu mwanamume amenitendea mambo mengi na nimemuachia Mungu amtendee

nilimpata kama hana chochote tukisonga na mbele ananirudisha nyuma," Serah alisema

 

Kwa mengi zaidi tembelea Radiojambo youtube.