logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho:Niliachana na mke wangu baada ya kuvuta uume wangu

Pia alikiri kuwa mume wake alikuwa anapenda wasichana sana na ni kichwa ngumu.

image
na Radio Jambo

Habari14 July 2021 - 05:38

Muhtasari


  • Bi Juliet aliuma ujumbe ili apatanishwe na mumewe, Macdonald ambaye waliachana miaka minne iliyopita
  • Juliet alisema kwamba walikuwa wameona kwa mwaka mmoja na nusu, na kubarikiwa na mtoto mmoja

Bi Juliet aliuma ujumbe ili apatanishwe na mumewe, Macdonald ambaye waliachana miaka minne iliyopita.

Juliet alisema kwamba walikuwa wameona kwa mwaka mmoja na nusu, na kubarikiwa na mtoto mmoja.

Pia alikiri kuwa mume wake alikuwa anapenda wasichana sana na ni kichwa ngumu.

"Niliachana na mume wangu kwa sababu alikuwa anapenda wasichana saana, mpaka alikuwa anataka kuwa na uhusiano na msichana wa kazi

Amekuwa akioa wasichana kisha wanaenda kwa maana hapendi kukaa na mwanamke mmoja,ntaka pia alee mtoto wetu

KUna wakati tulienda kwao nikapata ameoa mke mwingine, alikuwa ana lala nje, makosa yangu nilikuwa nampigia kelele sana," Juliet alisema.

Baada ya kufanya juhudi za kumfikia bwana Macdonald naye alikuwa na haya ya kusema.

"Huyu mwanamke amenifanyia mambo mengi sana, kuna wakati alikuwa anataka kuniua, pia alivuta uume wangu ndio tukaachana, amekuwa akiwatusi wazazi wangu

Amechukua pia hati zangu na kuficha,alikuwa pia anaenda kanisani kuwatusi wanawake wote ambao nilikuwa naongea na wao, alikuwa ananifuta mpaka jijini Nairobi ananivuta, nilitoka Nairobi nikaenda kukaa nyumbani kwa ajili ya hayo,"

Je nani wa kulaumiwa, kwa ajili ya kusambaratika kwa ndoa ya wawili hao? kwa uhondo zaidi tembelea Radiojambo Youtube.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved