logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho:Mke wangu aliniacha baada ya kumwambia twende tukaishi mashambani

Siku ya Ijumaa bwana KInyua alituma ujumbe ili apanishwa na mkewe

image
na Radio Jambo

Burudani16 July 2021 - 05:37

Muhtasari


  • Mke wangu aliniacha baada ya kumwambia twende tukaishi mashambani
  • Kila siku ya juma katika kipindi cha Gidi na Ghost asubuhi kitengo cha patanisho, wengi wamekuwa wakipatanishwa baada ya kukosana

Kila siku ya juma katika kipindi cha Gidi na Ghost asubuhi kitengo cha patanisho, wengi wamekuwa wakipatanishwa baada ya kukosana.

Siku ya Ijumaa bwana KInyua alituma ujumbe ili apanishwa na mkewe ambaye wamekuwa pamoja kwa zaidi ya miaka mitano, na walikosana miaka 6 iliyopita.

"Naomba mnipatanishe na mke wangu wa zaidi ya miaka 5. Tulikosana miaka 6 iliyopita. Tulikuwa tunaishi Nairobi na nikaamua twende nyumbani baada ya kazi yangu kuisha akakataa. Nikaenda na akaniletea mtoto baadaye

 nataka kumuomba msamaha kama nimemkosea, nataka tulee mtoto pamoja aliniachia mtoto ambaye nimekuwa nikimlea," Inyua Alisema.

Baada ya kufanya juhudi za umfikia mkewe alikuwa na haya ya kusema,

"Haiwezekani nishaaendelea na maisha yangu,"Mama Jim alisema.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved