- Niliachana na mke wangu baada ya kunipata na jumbe za wanawake
Katika kitengo cha patanisho bwana Daniel aliomba apatanishwe na mke wake, ambaye wamekuwa na yeye kwa miaka 4.
Kulingana na Daniel walikosana baada ya mke wake Catherine kumpata na jumbe za wanawake wa mitandaoni.
"Naomba nipatanishwe na mke wangu ambaye tumekuwa naye kwa miaka 4, tulikosana baada ya kunipata na jumbe za wanawake wengine mitandaoni
Ni mwanamke mzuri na nampenda ndio maana naomba kupatanishwa naye, nilikuwa naongea na wanwake wengine kwa maana alikuwa amenipa shiinikizo sana
Nakiri nitabadilika, na kuacha kuongea na wanawake," Daniel alisema.
Baada ya kufanya juhudi za kumfikia mkewe alikuwa na haya ya kusema kwa upande wake;
"Mimi sitaki kumuanika hewani, kwani alinikosea sana, nitamtafuta tuzungumze, kwa sasa nimekasirrika sana," Aliongea Catherine.
Je maoni yako ni yapi kuhusu patanisho ya leo?