logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho:Mke wangu aliniacha baada ya kunipata na jumbe za wanawake

Kulingana na Daniel walikosana baada ya mke wake Catherine kumpata na jumbe za wanawake

image
na Radio Jambo

Burudani26 August 2021 - 05:48

Muhtasari


  • Niliachana na mke wangu baada ya kunipata na jumbe za wanawake

Katika kitengo cha patanisho bwana Daniel aliomba apatanishwe na mke wake, ambaye wamekuwa na yeye kwa miaka 4.

Kulingana na Daniel walikosana baada ya mke wake Catherine kumpata na jumbe za wanawake wa mitandaoni.

"Naomba nipatanishwe na mke wangu ambaye tumekuwa naye  kwa miaka 4, tulikosana baada ya kunipata na jumbe za wanawake wengine mitandaoni

Ni mwanamke mzuri na nampenda ndio maana naomba kupatanishwa naye, nilikuwa naongea na wanwake wengine kwa maana alikuwa amenipa shiinikizo sana

Nakiri nitabadilika, na kuacha kuongea na wanawake," Daniel alisema.

Baada ya kufanya juhudi za kumfikia mkewe alikuwa na haya ya kusema kwa upande wake;

"Mimi sitaki kumuanika hewani, kwani alinikosea sana, nitamtafuta tuzungumze, kwa sasa nimekasirrika sana," Aliongea Catherine.

Je maoni yako ni yapi kuhusu patanisho ya leo?

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved