logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho:Mchana peupe nilimfumania na mwanamume mwingine kitandani

Kulingana na Peter wamebarikiwa na moto mmoja, na alimfumania na mwanamume mwingine.

image
na Radio Jambo

Burudani20 December 2021 - 05:47

Muhtasari


  • Katika kitengo cha patanisho bwana Peter 35 alituma ujumbe ili apatanishwe na mkewe Lydia ambaye wamekuwa kwa ndoa kwa miaka 2
Gidi na Ghost

Katika kitengo cha patanisho bwana Peter 35 alituma ujumbe ili apatanishwe na mkewe Lydia ambaye wamekuwa kwa ndoa kwa miaka 2.

Kulingana na Peter wamebarikiwa na moto mmoja, na alimfumania na mwanamume mwingine.

Huu hapa usimulizi wake;

"Naomba nipatanaishwe na mke wangu ambaye tulikosana naye mwaka huu mwezi wa Septemba, nilifumania na mwanamume mwingine ambaye ni rafiki yangu wa karibu kitandani

Nataka turudiane naye kwani tumetoka mbali naye, na licha ya yote nampenda na wala sijawahi kuwa na mpango wa kando, baada ya hayo tuligombana na akarudi kwao

Naomba afunge masikio awache kusikia mambo ya nje, nataka tuendelee na maisha," Alieleza Peter.

Baada ya kufanya juhudi zetu za kumfikia mkewe,hazikufua dafu kwani simu yake ilikua imezimwa.

Je ushauri wako kwa mwanamume huyu ni upi? Kwa mengi zaidi tembelea Radiojambo Youtube.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved