logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Aliniacha kwa sababu nilikuwa nahanya,'Mwanamume akiri na kufichua sababu ya mkewe kumuacha

KUlingana na bwana huyo, mke wake alimuacha kwa sababu alikuwa anahanya

image
na Radio Jambo

Habari26 January 2022 - 05:48

Muhtasari


  • Mwanamume akiri na kufichua sababu ya mkewe kumuacha

Bwana Alphonse,27,alituma ujumbe ili apatanishwe na mke wake ambaye wamekuwa pamoja kwa miaka 2.

KUlingana na bwana huyo, mke wake alimuacha kwa sababu alikuwa anahanya, na kuwa na wanawake wengi.

"Naomba nipatanishwe na mke wangu ambaye tulikosana naye mwaka jana baada yangu kuhanya na wanawake wengi, nimekuwa nikimbembeleza arudi nyumbani lakini ananiambia atarudi lakini harudi

Wazazi wake ndio wanakataa arudi nyumbani nimebadilisha tabia yangu na nimeokoka, na nampenda mke wangu sana," Alieleza Alphonse.

Baada ya kumfikia mkewe, alisema kwamba ni kweli alikuwa anahanya na ndio maana alimuacha.

"Ndio alikuwa na wanawake wengi ndio maana nilitoka kwenye ndoa,lakini nitarudi anipe tu muda mfupi nitarudi."

Je Bi Jeska anastahili kumrudia mumewe au anapaswa kumchunga zaidi?

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved