logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: "Akili haiko sawa, imekorogeka" Jamaa asononeka wiki moja baada ya kuachwa na mpenziwe

Peter alieleza kuwa ndoa yake ya mwaka mmoja unusu ilisambaratika baada ya mkewe kumshuku kuwa na mipango wa kando.

image
na SAMUEL MAINA

Vipindi30 June 2023 - 06:06

Muhtasari


  • •Gidi pia aliwashauri vijana dhidi ya kuwapenda wasichana wa takriban miaka 21 kwa roho yote.

Peter Shabaya ,32, kutoka Changamwe alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na mke wake Eunice Awori ,21, ambaye alikosana naye takriban wiki moja iliyopita.

Peter alieleza kuwa ndoa yake ya mwaka mmoja unusu ilisambaratika baada ya mkewe kumshuku kuwa na mipango wa kando. 

"Nikienda kwa nyumba nikiwa nimechelewa anauliza natoka wapi usiku. Namwambia ni sababu ya kazi. Alikuwa ananishuku niko na wasichana ila si kweli. Sikuwa na mpango wa kando. Sikuwa na msichana yeyote," Peter alisema.

Aliongeza, "Alikuwa ananishuku kwa sababu ya kuingia kwa nyumba usiku. Huwa nampigia simu lakini hatuelewani. Hata jana nilimpigia lakini hatukuelewana. Nasononeka sana hata mawazo ni mengi. Najiuliza mbona iko hivi."

Peter alisema mkewe alihamia kwa kaka yake baada ya kuondoka.

Kwa bahati mbaya, Eunice hakupatikana kwa simu wakati alipopigiwa na Gidi.

Peter alisema, "Hata jana tulikorofishana akaniambia anaweza kuzima simu. Kutoka jana akili yangu haiko kabisa. Akili yangu imekorogeka. Nimeshindwa hadi kuelewa. Nimechanganyikiwa kabisa. Niko kazini lakini ni kujaribu tu "

Peter alibainisha kwamba anampenda mama huyo wa mtoto wake mmoja kwa roho yake yote

Alipopewa fursa ya kuzungumza naye hewani alisema, "Eunice nakuomba rejesha roho yako chini tuongee. Sijawahi kukusea maishani, hii ni mara ya kwanza. Nakupenda na roho yangu yote. Nakuomba msamaha."

Huku akimshauri kuhusu jinsi ya kukabiliana na anayopitia, Gidi alimwambia Peter, "Usimpigie simu sasa hivi mpaka atakapotulia. Akitulia mtazungumza. Huenda bado amekasirika ndio maana mnakorofishana. Mpe muda atulie."

Gidi pia aliwashauri vijana dhidi ya kuwapenda wasichana wa takriban miaka 21 kwa roho yote.

Je, ushauri wako kwa Peter ni upi?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved