logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: Jamaa aachwa na mkewe mjamzito baada ya kumpiga, ajuta na kumlilia arudi

"Alisema hawezi kurudi. Hakunipa sababu," Kevin alisema.

image
na Radio Jambo

Habari12 September 2023 - 05:24

Muhtasari


•Kevin alisema mkewe ambaye ni mjamzito aliondoka bila ilani wakati akiwa kazini baada ya kumpiga kufuatia mzozo wa kinyumbani.

•Jaribio la kuwapanisha wawili hao hata hivyo liligonga mwamba kwani Lydia hakushika simu wakati Gidi alipompiga.

Kevin Moreka Nyangau ,26, kutoka Kisii alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na mke wake Lydia Kemunto ,21, ambaye alikosana naye miezi miwili  iliyopita.

Kevin alisema mkewe ambaye ni mjamzito aliondoka bila ilani wakati akiwa kazini baada ya kumpiga kufuatia mzozo wa kinyumbani.

"Nilikuwa na simu. Ilikuwa imeharibika. Yeye ndo alikuwa ameharibu. Nikaamua niuze ninunue ingine. Hiyo ndo ilileta shida. Nilipomwambia nimeuza alianza kunitusi. Nilikasirika nikampiga kofi. Baada ya kumpiga niliomba msamaha. Nilitoka nikaenda shughuli zangu. Kumbe alikuwa amepanga kuenda," Kevin alisimulia.

Aliendelea, "Nimejaribu kuongea na yeye akasema nimtumie nauli arudi. Baadaye alikasirika akasema nisitume hatarudi. Tulikuwa tumeogea Ijumaa, alisema nitume Jumamosi ndio arudi Jumapili ama Jumatatu. Jioni alibadilisha wazo akasema nisitume hatarudi. Huwa naongea na mama yake. Alisema hajamuona nyumbani. Ako kwa dadake."

Kevin alisema ilikuwa mara ya kwanza kumpiga mkewe.

"Alisema hawezi kurudi. Hakunipa sababu," Kevin alisema.

Jaribio la kuwapanisha wawili hao hata hivyo liligonga mwamba kwani Lydia hakushika simu wakati Gidi alipompiga.

Kevin alipopewa nafasi ya kuzungumza na mkewe hewani alisema, "Babe najua nilikosea. Ningetaka kujua mahali ulienda. Bado nakupenda. Ningependa urudi."

Je, una ushauri gani kwa Kevin?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved