logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: “Nahitaji damu!” Mke mgonjwa amsuta mumewe akiwa hospitalini kwa kutomtembelea

"Nauli ya kufika huko ndio sina.Vile alikuwa anagonjeka tulikuwa na yeye." Charles alijitetea.

image
na SAMUEL MAINA

Vipindi10 November 2023 - 06:10

Muhtasari


  • •Charles alisema ingawa bado hawajatengana, mkewe alienda kwa dadake akiwa na ujauzito wa mtoto wao wa kwanza pamoja ila bado hajaweza kurejea miezi miwili baadaye.
  • •Mama Ronnie alidhihirisha kuwa yupo hospitalini ambapo anaendelea kupokea matibabu na Bw Charles bado hajapiga hatua ya kumtembelea.
GHOST NA GIDI STUDIONI

Jamaa aliyejitambulisha kama Charles Martin Mundia mwenye umri wa miaka 24 kutoka Vihiga alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na mke wake Mama Ronnie ,25, ambaye amekuwa mbali naye kwa miezi miwili.

Charles alisema ingawa bado hawajatengana, mkewe alienda kwa dadake akiwa na ujauzito wa mtoto wao wa kwanza pamoja ila bado hajaweza kurejea miezi miwili baadaye. Alisema mkewe alikuwa mgonjwa wakati aliondoka.

"Alikuwa mgonjwa akasema anaenda kwa dada yake kupata matibabu lakini hajarudi. Tuliongea na yeye hata jana lakini hatukuelewana vizuri. Nikimwambia arudi anasema ningoje, nashangaa atarudi siku gani. Bado hajapona lakini saa hii ako poa kidogo," Charles alisema.

Aliongeza, "Nilimuuliza makosa yangu akasema sina makosa yoyote kwake. Kwao bado sijajitambulisha rasmi lakini tumeongea na mama yake kwa simu. Miezi mbili nimekaa nimengoja harudi."

Wakati Mama Ronnie alipopigiwa simu, alizungumza kwa sauti nyonge, ishara kuwa alikuwa anakabiliana na maumivu.

Alidhihirisha kuwa yupo hospitalini ambapo anaendelea kupokea matibabu na Bw Charles bado hajapiga hatua ya kumtembelea.

"Niko hospitali. Ata yeye (Charles) anajua, anajifanya hanijui. Hajakuja kuniona. Tangu nigonjeke hajakuja kuniona," alisema.

Aliongeza, "Nilikuwa nataka damu ili niongezwe mwili. Bado hajakuja. Ata nimemwambia mara mingi hataki kuja."

Charles alijitetea kwa kusema, "Nauli ya kufika huko ndio sina.Vile alikuwa anagonjeka tulikuwa na yeye."

Watangazaji Gidi na Ghost Mulee walimsuta sana jamaa huyo kwa kutopiga hatua ya kumuona mkewe mgonjwa hospitalini na kumuagiza kufanya vile mara moja kabla hata ya mikakati ya kurudiana kuanza.

Je, una maoni yapi kuhusu Patanisho ya leo?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved